Kamati ya saidia timu ya taifa ya
vijana chini ya umri wa miaka 17 Serengeti Boys imeshangazwa na utaratibu wa
makato ya fedha zilizopatikana mara baada ya mashabiki kujitokeza katika uwanja
wa taifa jijini Dar es salaam wakati wa mchezo wa kwanza kati ya timu hiyo
dhidi ya timu ya taifa ya Kongo Brazzaville uliochezwa mwishoni mwa juma
lililopita.
Katibu wa kamati hiyo Henry Tandau amesema makato ya fedha
zilizopatikana yamewashangaza kutokana na dhana ya utaifa kuwekwa nyuma na
badala yake kuiacha kamati yao na harakati nzito za kuendelea kuisaidia
Serengeti boys.
Msikilize Tandau akiishukia TFF juu ya mapato
0 comments:
Post a Comment