
Moja kati ya matuki ya makubwa ya Ngasa katika soka.
Baba mzazi wa mshambuliaji wa Simba Mrisho Ngasa ambaye kwa
sasa ni kocha wa klabu ya Polisi Iringa
na Khalfani Ngasa amefunguka juu ya kutotazamwa vizuri na mwanae katika mambo
mbalimbali yanayomuhusu katika maisha yake.
Akizungumza na Mwananchi Ngasa amesema yanayozungumzwa kuhusu
mtoto wake si yakweli na anamtimizia kila anachokitaka. “Ngasa ni mwanangu
nashukuru naishi naye vizuri ananiheshimu nami na muheshimu, hajawahi kunitolea
hata neno moja la kijeuri tangu pale alipoanza kupata jina katika medani ya
soka na kuhusu msaada ananisaidia pale kwa wakati bila ya matatizo yoyote” Mzee
Ngasa alisema hivyo.
Aidha mzee Ngasa amekana kauli za wadau wanaodai kuwa Mrisho
ameshuka kiwango kutokana na kuwa na wake watatu kama inavyoruhusiwa imani yake
ya kiislamu, amesema si kweli Ngasa hana wake wa tatu zidi ya mmoja aliemuoa
miaka michache iliyopita na hajakubaliana na suala kushuka kiwangp cha mwanae
huku akisema kwamba mchezo wa soka unaendana na sera ya timu kwa hiyo nivugumu
kwa mchezaji kukopi iana timu mapema mno.
Kuhusu kipaji cha Ngasa amesema yeye alitarajia kuwa mtoto
wake angefika hapa alipo sasa kutokana alipita katika mikono yake akiwa kama
kocha,kwenye kituo maarufu cha soka cha
Channel Africa,kilichopo jijini Mwanza wilaya ya Ilemelea, akiwemo ngasa na
nyota wengine kama Henry Joseph aliopo Sweden akicheza soka la kulipwa.
0 comments:
Post a Comment