SHUJAA WA KWANZA IRINGA, AFUNGUKA JUU YA SOKA MKOA HUO.



                      
      Shujaa alieipandisha Lipuli mwa 1991 Chachage Bukaza.
Nyota wa zamani wa timu ya Lipuli ya Iringa Dr.Chachage Bukaza kutokuwepo kwa nguvu ya makampuni yanayomiliki na kusimamia vilabu soka la Iringa haliwezi kusimama kwenye mstari wa zamani wa ushindani katika soka.
Bukaza ambaye kwa sasa na muhadhiri wa chuo kikuu cha Tumaini kilichopo mkoani Iringa huku akiwa na historia kubwa ya soka mkoani Iringa ambapo mwaka 1991 Chacha alifunga goli pekee lililo iwezesha Lipuli kupanda kwa mara ya kwanza ligi kuu ya Tanzania bara.
Amesema tatizo kubwa la kudumaa kwa soka mkoani Iringa ni kukosekana kwa fedha na watu wakutazama mchezo huku akielezea kipindi cha nyuma wao walikuwa wakifanya makubwa kutokana walikuwa wakitazamwa na kupata kila wanacho kihitaji katika timu zao.
Aliongeza pia kuwepo kwa timu za Retco, Pareto, Chai na makampuni kulichangia kuwepo kwa mafanikio ya soka kwa wakati huo.
Wakati huo huyo katibu wa chama cha soka mkoani Iringa Eliud Mvela amesema lazima wadau watoboe mifuko yao kuchangia soka ikiwemo timu ya Polisi Iringa ambayo kwa sasa inawania nafasi ya kupanda ligi kuu ya Tanzania bara, amesema wadau wapo wengi ila ni viongozi wa lawama kuliko kuchangia na kutaka kutambua hali ya vilabu vinavyowakilisha mkoa.
Soka la Iringa limepotea kwenye ramani ya kitaifa kwa maana ya ligi kuu ya Tanzania bara tangu mwaka 1999 iliposhuka daraja kutoka ligi kuu ya Tanzania.

0 comments:

Post a Comment