WATANO WALIONGIA KWENYE KIKAO CHA UBORA WA BBC.



           Demba Ba, Younes Belhanda, Didier Drogba, Christopher Katongo and Yaya Toure
                               Majembe yanayo wania tuzo.
Shirika la utangazaji la BBC limetoa orodha ya majina matano ya wachezaji watakaowania uchezaji bora wa Afrika kwa tuzo za BBC.
Wachezaji wamepangwa kama ifuatavyo ambapo mchezaji bora wa Africa kwa mwaka wa 2011 Yaya Toure na Didier Drogba wote wa Ivory Coast wa Msenegal Demba Ba , Mmorocco Younes Belhanda and Mzambia Christopher Katongo. Ndio watakaowakilisha katika tuzo hizo
Wakati kura zitaanza kupigwa December 13. Lakini kama wadau wanapswa kuchagua mchezaji bora kwa nambari +44 7786 20 50 75:  na mshindi kutangwa December 17
Namba za washiriki hao ni.
Text 1 for Demba Ba,Text 2 for Younes Belhanda ,Text 3 for Didier Drogba
Text 4 for Christopher Katongo, Or Text 5 for Yaya Toure
DROGBA. Uwezo mkubwa alio uonesha kwenye michuano ya klabu bingwa na kule nchini Ujerumani na kuifanya Chelsea kutwaa taji la mabingwa barani ulaya lakini alifunga goli lililoiwezesha timu ya Chelsea kutwaa kombe la FA.
YAYA TOURE. Sababu alikuwa ndiyo funguo ya Manchester City msimu uliopita na kuiwezesha timu kutwaa ubingwa wa England kwa 2011/2012 baada ya ukame wa miaka takribani 44.
YOUHANES BELHANDA. Akiwa na klabu ya Montele ya nchini Ufaransa alishiriki kikamilifu huku akipachika magoli 12 na kutwaa ubingwa wa Ligi one
FELIX KATONGO. Nyota huyu akiwa kama nahodha alikiwezesha kikosi cha Zambia kutwaa taji la Africa kwa mwaka wa 2012 baada ya kufunga Ivory Caost.
DEMBA Ba. Akiwa kama nyota wa Newcastle united msimu uliopta alikiwezesha kikosi chake kumaliza nafasi ya tano kwenye ligi England huku akiwa na magoli 17 wakati msimu huu anashika nafasi ya pili akiwa na magoli 8.

Mwaka 2011 mshambuliajiwa Ghana naOlimpic Marselle, Ayew Pelle alitwaa tuzo hiyo.

TANDAU AISHUKIA TFF JUU YA MAPATO.



Kamati ya saidia timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 Serengeti Boys imeshangazwa na utaratibu wa makato ya fedha zilizopatikana mara baada ya mashabiki kujitokeza katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam wakati wa mchezo wa kwanza kati ya timu hiyo dhidi ya timu ya taifa ya Kongo Brazzaville uliochezwa mwishoni mwa juma lililopita.

Katibu wa kamati hiyo Henry Tandau amesema makato ya fedha zilizopatikana yamewashangaza kutokana na dhana ya utaifa kuwekwa nyuma na badala yake kuiacha kamati yao na harakati nzito za kuendelea kuisaidia Serengeti boys.

Msikilize Tandau akiishukia TFF juu ya mapato

BENITZ AINGIA KWENYE KIKOSI CHA MAJANGILI.



 Rafael Benitez
    Huyu ndiye Benitez aliyekabidhiwa mfupa uliyemshinda Fisi.
Masaa kadhaa baada ya kumfukuza aliyekuwa kocha wake Roberto Di Matteo uongozi wa klabu ya Chelsea umemteua kocha wa zamani wa klabu ya Liverpool Rafael Banitez kuziba nafasi hiyo hadi mwishoni mwa msimu huu.
Benitez mwenye umri wa miaka 52 mara baada ya kutangazwa kuchukua nafasi hiyo anatarajiwa kukutana na mmiliki wa Chelsea Roman Abromovich ilikumalizana naye katika baadhi ya mambo mhimu.
Kwamujibu wa taarifa iliyotolewa kwenye mtandano wa klabu hiyo imeeleza kuwa mmliki wamabingwa hao wa ulaya kwa upande wa vilabu na bodi ya wakurugenzi wanaimani kuwa Benitez ni chaguo sahihi kwakuwa anauzoefu wa kutosha.
Benitez aliyefukuzwa na Inter Milan december mwaka 2010 baada ya kuifundisha timu hiyo kwa miezi sita anatarajiwa kuhudhuria mazoezi ya timu yake mpya leo.
Benitez anakuwa kocha wa 9 kushika nafasi hiyo ndani ya klabu ya chelsea tangu inunuliwe na bilionea huyo raia wa Urusi mnamo mwaka 2003.

DI MATEO NJE CHELSEA



                      File:Dimatteo2 cropped.jpg
Uongozi wa klabu ya Chelsea umemfukuza kazi menejea wake Roberto Di Matteo baada ya kuitumikia klabu hiyo takribani kwa miezi minane na kuipatia mataji mawili ya FA Cup na ligi ya mabingwa barani ulaya.
Kwamujibu wa taarifa toka kwenye mtandao wa klabu hiyo Di Mateo amefukuzwa kazi baada ya kikao cha bodi na mmiliki wa klabu hiyo na kilicho jadili hatma ya meneja huyo na kutoridhika na utendaji wake haswa kwa matokeo ya hivi karibuni.
Bodi hiyo imemshukuru  Di Mateo kwa alichokifanya kwa kipindi chote haswa kuleta taji kubwa barani ulaya la ligi ya mabingwa alipoifunga Bayern Munich kwenye  mchezo wa fainali mei 19 mwaka huu.
Matokeo mabaya ya ligi ya mabingwa yaliyopoteza matumaini ya kutetea ubingwa wa ulaya na yale ligi kuu ya England yaliyoitoa timu hiyo kileleni hadi nafasi ya tatu yameonekana kuwa chanzo mbali na kucheza soka la kuvutia linalotakiwa na mmiliki wa klabu hiyo.
Di Mateo mwenye umri wa miaka  42 aliwahi kuichezea timu hiyo kuanzia mwaka 1996 hadi 2002 na juni 13 mwaka huu alipewa mkataba wa miaka miwili kama meneja wa timu hiyo baada ya kukaimu vema nafasi ya aliekuwa kocha wa timu hiyo Andres Vila Boas.
MWISHO.
Mameneja waliopita tangu Roman Abramovich ainunue Chelsea.
  • Claudio Ranieri: Sep 2000 to May 2004
  • Jose Mourinho: Jun 2004 to Sep 2007
  • Avram Grant: Sep 2007 to May 2008
  • Luiz Felipe Scolari: Jul 2008 to Feb 2009
  • Guus Hiddink: Feb 2009 to May 2009
  • Carlo Ancelotti: Jun 2009 to May 2011
  • Andre Villas-Boas: Jun 2011 to Mar 2012
  • Roberto Di Matteo: Mar 2012 to Nov 2012

MVELA AWAONDOA HOFU WADAU JUU YA KESI YA RUSHWA.



              
                       Katibu wa IRFA Eliud Mvela.
Siku chache baada ya kupelekwa mahakani kwa tuhuma za rushwa katibu wa chama cha soka mkoani Iringa  Eliund Mvela amewataka wadau wa soka mkoani humo kuondoa hofu juu  ya kesi yake na kudai kuwa shughuri za soka zitaendelea kusonga kama kawaida kwa ushirikiano wake na wadau wa soka.
Akizungumza na mwananchi Mvella ambaye pia ni katibu wa kamati ya utendaji ya shirikisho la soka nchini Tanzania TFF amekataa kudhihirisha kama ni kweli alitoa rushwa ama hakutoa, kwa kusema kwa kuwa kesi ipo mahakani basi iachiwe mahakama kufanya maamuzi yake.
Mwishoni mwa juma lililopita Mvela alifikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Mfawidhi kusomewa shitaka linalomkabili la rushwa ambapo kamanda wa TAKUKURU Mkoani iringa Emma Kuhanga alithibitisha kuwa Mvela ameshtakiwa lwa kifungu cha 15. 1b kifungu cha sheria namba 11 cha mwaka 2007.
katika taarifa yake Kuhanga alisema mnamo tarehe 27 Septemba 2012 katika maeneo ya Kihesa Ngome, mtuhumiwa akiwa mgombea wa CCM alimpa Katibu wa chama hicho Kata ya Kihesa Yusuph Mabena shilingi elfu 70 ambayo igawanywe kwa wana CCM waliokuwa wamekusanyika katika nyumba ya Anna Myinga ikiwa kama kishawishi kwao ili waweze kumpigia kura katika nafasi aliyokuwa akigombea.

mbali na harakati hizo  za utoaji rushwa katika uchaguzi wa CCM mkoa uliofanyika Septemba 28, mwaka huu, Mvela alikuwa mgombea wa nafasi ya uenyekiti wa wilaya hakufanikiwa kushinda kutokana na kuandamwa kwa rushwa.
 Kwa mujibu wa kifungu hicho, Mtuhumiwa wa makosa kama hayo endapo atashindwa kesi atatakiwa kulipa faini kati ya shilingi laki tano na milioni moja au kutumikia jela kati ya muda wa miaka isiyopungua 3 na isiyozidi 5.
 Kesi hiyo inasikilizwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa ambapo itaanza kusikilizwa Desemba 13, mwaka huu.
kutokana na kesi hiyo wadau waliowengi wamekuwa na shaka ikiwemo kuondoa imani ya kiongozi wao wa soka ambaye anadhima kubwa ya kiutendaji katika soka la Iringa.