YANGA YAENDA DODOMA.

                               Yanga ilivyotinga bungeni mwaka 2011 baada ya kutwaa ubingwa.

Klabu ya soka ya Yanga imesafiri mchana wa leo kulekea mjini Dodoma tayari kwa kuringisha kombe lake la Kagame ambalo wamelitetea kwa mara ya pili na kulibakisha nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa msemaji wa Yanga Luis Sendeu amaesema baada ya ziara hiyo Yanga itarejea Dar kwa maandalizi zaidi ya ligi kuu ya Tanzania bara.

Hapo jana klabu ya Yanga imemtambulisha rasmi mshambuliaji wake mpya Didier Kavumbagu aliesajiliwa na mabingwa hao wa Kagame julai 28 mwaka huu akitokea klabu ya Atretico ya Burundi.

0 comments:

Post a Comment