NGASA KUGOMA KWENDA SIMBA.


Usajili wa Mrisho Ngasa ndani ya klabu ya Simba bado ni kitendawili hii ni baada ya nyota huyo kuonekana kutokubaliana na maamuzi ya Azam FC kumuuza mchezaji huyo bila ya makubaliano nay eye binafsi .

Habari iliyojificha inasema kuwa nyota huyo alikutwa akitamka kuwa hata yeye mwenyewe ana ubavu wa kujiununu na yupo radhi kuvunja mkataba au kubaki Azam hadi mkataba wake umalizike na ajiunge na klabu anayoipenda.

Kwa upande wa uongozi wa Yanga, kupitia msemaji wake Luis Sendeu wanaimani kuwa wata mnyakua mshambuliaji huyo bila ya malipo yoyote kwa kuwa na imani Ngasa bado ni mali yao katika medani ya soka la Tanzania.

Ngasa aliuzwa kwa mkopo mchana wa jana kwa dau la shilingi milioni 25 kwa makubaliano ya pande mbili kati ya uongozi wa Simba na Azam fc. Huku taratibu zikidaiwa kukiukwa kwa kuwa Ngasa hakushirikishwa katika hilo.

Tukio hili linakwenda sambamba na lile la nyota wa zamani wa Simba, Mohammed Banka, Meshack Abel walipotaka malipo yao baada ya Simba kutaka kuwauza kwa mkopo. Lakini Julias Mrope wa Yanga alipokataa kuzwa Moro kwa mkopo.

0 comments:

Post a Comment