SIMBA YAKARIBIA KUMNUNUA NGASA, HUKU KOCHA AKIFUANGIWA VIRAGO VYAKE.


Uongozi wa klabu ya Azam umekana taarifa za kumuuza mchezaji abubakary Salum Sure Boy .
Hayo yamesemwa na kutihibisha mchana wa leo na msemaji wa Azam Japha Iddi Maganga baada ya kusambaa kwa taarifa za kufukuzwa kwa kocha wa timu hiyo raia wa England.

Maganga amesema suala la kufuukuzwa kocha ni kweli kocha ametisitishiwa mkataba wake na nafasi yake imeshikwa na kocha msaidizi Kally Ongala huku upande wa Sure Boy klabu hiyo haijatangaza chochote juu ya mauzo ya nyota huyo.

Kwa upande wa mshambuliaji wake Mrisho Ngasa anayesadikiwa kutakiwa na klabu ya jangwani huku yeye mwenye akionyesha mapenzi na timu hiyo haswa katika michuano iliyopita ya Kagame ambapo Ngasa alivalishwa jezi ya Yanga na mashabiki naye kuibusu bila ya woga, Maganga amesema nyota huyo ametangaziwa ofa yake kuwa ni  dola 50,000  za kimarekani ikiwa na maana klabu yoyote ikiwa tayari ruksa kuuziwa.

Hadi Blogu hii inaondoka kwenye maskani ya Azam klabu ya Simba ndiyo iliyokuwa ikisadikiwa kuwa inaweza ikafanya biashara na wana rambaramba wa Azam FC.

Sure boy na Ngasa walidaiwa na mashabiki kuwa walicheza chini ya kiwango kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Yanga huku kocha akidaiwa na wadau hao kwamba alifanya kinyume kumchezesha Ngasa kwenye mchezo wa fainali.

0 comments:

Post a Comment