Fainali ya kombe la Politani Cup imelazwa hii leo na kusuburi tarahe nyingine baada ya mchezo huo uliowakutanisha Wangongo na Sateta kumalizika kwa sare ya magoli mawili kwa mawili.
Katika mchezo huo Wangongo walikuwa wakwanza kufunga baada ya mshambuliaji wake Nassor Saidi maarufu kama Choro kufunga goli kwa faulo yenye ufundi wa hali ya juu, hadi kipindi cha kwanza kinamalizika Wangongo walikuwa wababe wa Sateta.
Katika dakika za mwisho za mchezo huo timu ya Sateta ilimudu kuchomoa goli hilo kupitia Amos Mgisa na baadae kufunga goli la pili lilifungwa na Adam Kingwande na kufunika matumaini ya mashabiki wa Wangongo waliokuwa na uchu wakutaka kufuturu wakiwa mabingwa wa kombe hilo.
Dakika sita baadaye Sateta walipachika goli la 2 na kusawazisha kwa kuweka sare ya magoli mawili kwa mawili.
Dakika tano baadaye mwamuzi Omary alimaliza mchezo huo na kupatika maamuzi ya kuahilishwa kwa pambano na waandaji wa pambano kitendo ambacho hakikupendwa na mashabiki wengi.
Kwa mujibu wa waandaji wa mashindano hayo imeelezwa kuwa mchezo huo huenda ukarudiwa jumapili ijayo baada ya mazungumzo na timu zote mbili.
0 comments:
Post a Comment