HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA, NGASA KATUA RASMI SIMBA.


Mshambuliaji nguli wa timu ya Azam na timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars ametangazwa rasmi kuwa mchezaji mpya wa klabu ya Simba kwa mkopo baada ya klabu ya Azam kukubali kupokea ofa ya shilingi milioni 25 toka kwa wekundu hao.

Ofa hiyo iliyotangazwa kwa takribani siku nne tangu mchezo wa fainali umalizike ambapo mauzo hayo yalizingatia tamaa ya kuitaka kuichezea klabu yake ya zamani ya Yanga.

Kwamujibu wa taarifa zilizopo chini ya Kapeti zinasema kuwa mshambuliaji huyo amegoma kwenda Simba na sasa yupo kwenye mipango ya kurudi kwao mwanza kupumzika.

Kiasi  cha dola elfu hasmini za kimarekani zilitangazwa kama dau la mauzo ya moja kwa moja kwa nyota huyo mahiri wa Azam.

0 comments:

Post a Comment