CHOMBO AFUNGUKA JUU YA MKATABA WAKE NA SIMBA


Aliyekuwa mchezaji wa Azam Fc Ramadhani Chombo Ridondoo leo ameweka wazi kuhusu mkataba wake mpya aliosaini jana kuchezea simba msimu huu.

Chombo amesema mkataba wake na Azam umemalizika mwezi juni mwaka huu na alikuwa na ugomvi mkubwa na klabu hiyo ambapo alifungiwa kwa muda wa miezi minne bila kulipwa mshahara .

Amesema amesugua benchi kusubiri mkataba mwingine lakini hakukuwa na hata kiongozi wa kumuongeza matokeo akasaini na Simba.

Hapo jana kiungo huyo wa kitanzania mwenye sifa ya kufanya vitu vya ajabu akiwa uwanjani alisaini mkataba wa miaka miwili na klabu ya Simba kwa dau la shilingi milioni 30.

0 comments:

Post a Comment