Haya ni makubwa mno yaliyotokea kwenye uwanja wa taifa baada ya vichapo vitatu kuikumba Yanga toka kwa Azam FC hii leo wana jangwani ikiwa ni siku kumi na tatu tangu kupata uongozi mpya Yanga yavunja uteja kwa Azam baada ya kufinga magoli 2 kwa 0 na kutwaa taji la Kagame Cup 2012.
Kwa ushindi huo Yanga imechora ramani ya mpya ya kutwaa taji hilo ma mbili mfululizo ikichagizwa na msimu uliopita ambapo Yanga ilitwaa ubingwa huo mbele ya Simba baada ya kushinda goli moja lilifungwa na Keneth Asamoh kwa kuitumia pasi safi ya rashidi Gumbo.
Kabla ya kuanza kwa pambano hilo yanga tayari ili ahidiwa kiasi cha million 30 kama posho ya kuichapa Azam FC.
0 comments:
Post a Comment