YONDANI NJE WIKI MBILI.



                
                   Yondani akiwa na jezi ya Yanga.
Taarifa yenye kusikitisha kwa mashabiki wa klabu ya soka ya Yanga kuwa mlinzi wa klabu hiyo Calvin Yondani amepasuka mfupa wa mguu wake wa kulia baada ya kugongwa na kiungo wa Simba Haruna Moshi Boban katika mchezo wa ligi kuu uliochezwa juzi kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Blog hii daktari wa timu ya Yanga Juma Sufiani amesema kuwa jeraha hilo litamgharimu takribani wiki zisizo pungua mbili kukaa nje ya uwanja kwaaji ya matibabu zaidi.

Sufiani amesema maumivu ya mchezaji huyo ni makubwa kiasi ambacho anatembelea magongo maalum kwaajili ya kumpa nguvu ya kusogea kutoka sehemu moja hadi nyingine.

Kuumia kwa Yondani kunatukumbusha  mengi yaliyopoteza viwango vya nyota wetu kama ilivyokuwa kwa Victor Costa wa aliekuwa samba kipindi hicho na uhuru Selemani wa Simba, Shamte Ali wa yanga ambaye bado wanalitumikia soka la Tanzania.

0 comments:

Post a Comment