RONALDO KUCHEZA URENO.



            
Mashambuliaji wa Real Madrid Cristian Ronaldo, ameruhusiwa kuitumikia timu yake ya taifa ya ureno, katika mchezo wa kimataifa kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia mwaka 2014 kule nchini Brazil.
Ronaldo amepewa ruhusa hiyo na jopo la madaktari wa klabu yake ya Real Madrid baada ya kugundulika kuwa amepona jeraha la bega alilolipata katika mchezo wa jumapili dhidi ya Barcelona.
Baada ya sare ya magoli kwa 2 kwa 2 ya El Classico, kocha wa timu ya taifa ya Ureno Paul Bento alikata tama ya kumtumia mchezaji huyo baada ya kusikia ameumia bega mbalina kumaliza dakika zote 90.
Oktoba 12 kikosi cha Ureno kitakuwa ugenini mjini Moscow kucheza na timu ya taifa Urusi katika mchezo huo wa kuwania tiketi ya kufuzu fainali za kombe la dunia 2014. 

0 comments:

Post a Comment