Kamati
ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF, imetupilia mbali
rufani iliyowasilishwa na warufani Mussa Mahundi, Abou Silia na Alex Mgongolwa,
dhidi ya kamati ya uchaguzi ya chama cha mpira mkoani Iringa
IRFA.
Warufani hao waliokuwa wakiwania nafasi za uongozi wa soka mkoani Iringa
waliitaka kamati ya TFF, kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa IRFA, uliofanyika
September 8 mjini Mufindi, sambamba na kuomba uchaguzi ufanyike upya chini ya
kamati ya uchaguzi ya TFF.
Baada ya kupitia rufaa hiyo, mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi ya TFF,
Deogratius Lyato ameeleza kuwa rufaa hiyo imekosa sifa ya kamati yake kwa
mujibu wa kanuni za uchaguzi za TFF ibara ya kwanza 8 (2) ibara 21(3) na ibara
ya 24(2) kwa kutozingatia matakwa ya kanuni za chaguzi za wanachama wa
TFF.
Lakini pia Kamati ya Uchaguzi ya TFF imeiagiza Kamati ya Uchaguzi ya IRFA
kuchukua hatua dhidi ya mdau wa michezo, Abuu Changawa kama ilivyoainishwa
kwenye Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF, Ibara ya 28(6) kwa kuingilia
mchakato wa uchaguzi wa IRFA siku ya uchaguzi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment