FARG AWAPOKEA ROONY NA FLETCHER




Kocha wa Manchester united Sir Alex Ferguson amewakaribisha kwa pongezi kubwa nyota wake Wayne Roony na Darren Fletcher kwa kurejea uwanjani kwa kuiletea klabu mafanikio makubwa katika mchezo wa kwanza wa kombe la ligi.
Katika mchezo Fagason alivutiwa na viwango vya wachezaji wake akiwemo Roony alieonekana jana kwa mara ya kwanza tangu alipoumia mguu katika ushindi wa magoli  3 kwa 2 dhidi ya Fulham.
Kwa upande wa nahodha wa Scotland, Darren Fletcher ulikuwa ni mchezo wake wa kwanza aliposhindwa kuitumikia klabu hiyo tangu mwaka 2011 kutoka na kusumbuliwa na matatizo ya tumbo.
Fagason amesema kuwa sasa wanahitaji kuendeleza wimbi la ushindi katika mashindano yote yanayo endelea huku akisisitiza kuwa watashinda kila mchezo muhimu wa klabu hiyo.
Kwa upande wa wapinzani wao wa jana Newcastle United kupitia kocha wake Alan Pardew ameridhishwa na kurejea kwa mshambulaji wake Pappis Demba Cisse aliekuwa akisumbulia na kifundo cha mguu.
Katika mchezo huo wa jana Cisse alimfunga goli la kufutia machozi katika dakika ya  62.

0 comments:

Post a Comment