Siku moja baada ya kamati ya uchaguzi ya TFF kutangaza
kutupilia mbali rufani ya wagombe wa nafasi za uchaguzi mkoani humo Mussa
H.Mahundi, Abou O.Silia pamoja na mwanasehria Alex Mgongolwa, wadau wa soka
mkoani Iringa wamewataka viongozi wa soka kushirikiana katika kulikuza soka la
mkoa huo.
Akizungumza na Mwananchi mdau wa mchezo huo Juma Mpiluka
amesema kwa sasa kilichobaki ni kuacha
malumbano na kushirikiana na uongozi wa IRFA ilikujenga sura bora ya soka la
Iringa lililo poteza dila ya kitaifa tangu mwaka 1999 timu ya Lipuli ya Iringa
Iliposhuka daraja.
Mdau huyo aliongeza kuwa ni vema uongozi huo mpya chini ya mwenyekiti wake Cyprian
Kuyawa kuitisha mkutano wa wadau wa michezo ili kukusanya mawazo chanya
yatakayoweza kuleta mabadiliko katika soka la Iringa. Sambamba na kuutaka
uongozi uwateue wagombea walioshindwa katika kamatii mbalimbali za uongozi ili
kupata fursa ya kutumia mawazo na sera zao zilizo shindwa kufua dafu kwenye
uchaguzi.
Kwa upande wa mdau mwingine alikataa kutajwa jina lake alisema
kuwa suala la kushindwa kwa rufani hilo lilikuwa lipo wazi kutokana nguvu ya
katibu wa chama soka mkoani Iringa Eliudi Mvela ambaye pia ni mjumbe wa kamati
ya utendaji TFF taifa kuwa tayari cheo chake kinaweza kutoa maamuzi huku kanuni
ikipindishwa, sema kilichobaki ni kuongeza mshikamano wa nguvu kwa wadau wote
wa Iringa na kuboresha mchezo huo.
Kwa sasa mkoa wa Iringa na IRFA una kazi kubwa ya kuhakikisha
timu za Kurugenzi ya Mufndi na Polisi Iringa zinapanda ligi kuu msimu unaokuja.
Kumbuka kuwa katika uchaguzi uliofanyika September 8 kule
wilayani Mufindi, wajumbe wa IRFA waliwapitisha Cyprian Kuyava katika nafasi ya
uenyekiti, Stanford Mwakasala Makamu mwenyekiti, kwa upande wa katibu mkuu
Eliud Mvela alierudi madarakani kwa awamu ya tatu, Abwene Mwakalobo katibu
msaidizi,
Katika nafasi ya muhazini alichaguliwa Abdalah Kiyumbo,
Coasta Magoroso akirudi katika nafasi ya uwakilishi wa vilabu, Ramadhani Mahano
Mjumbe mkutano mkuu wakati waliochaguliwa kwenye kamati ya utendaji ni Maulidy
Toffy pamoj na Festor Mwamalekela.
0 comments:
Post a Comment