UEFA KUZIPIGA RUNGU UJERUMANI NA URENO


 
  Hapa kazi tu
Shirikishola soka barani Ulaya  Uefa limepanga kuviadhibu vyama vya soka vya mataifa ya Ujerumani na  Ureno kufuatia  matukio mawili yaliyotendwa kwenye mchezo wa nchi hizo kuwania kombe la mataifa ya Ulaya huko Poland na Ukrain.

 Uefa imesema kuwa chama cha soka cha Ujerumani kinakabiliwa na kesi ya mashabiki wake kutupa makombora  uwanjani wakati wenzao wa  Ureno  wakikabiliwa na adhabu kufuatia timu yao ya taifa kuchelewa kurudi uwanjani kipindi cha pili cha mchezo huo ambao Ujerumani ilishinda goli 1 kwa 0.

Taarifa hiyo imebainisha kuwa kamati ya nidhamu ya Uefa inataraji kukutana alhamisi ya juma hili kujadili juu ya sakata hilo ambalo limekuja  ikiwa ni siku chache tuu  baada ya mashindano hayo kuanza.

0 comments:

Post a Comment