MIRAJI KIKWETE ATEULIWA KUWA MAKAMU WA RAISI WA IBF



Shirikisho la Ngumi la Kimataifa Africa (IBF/Africa) limemteua ndugu Miraji Mrisho Kikwete kuwa Makamu wa Rais anayeshughulikia maendeleo ya vijana katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati hukua akisisitiza kuwa uteuzi huo unaanza utekelezaji wake mapema mwezi huu.
 
Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati, Onesmo Ngowi amesema kuwa Miraji ana uwezo wa kuwahamasisha na kuwaunganisha vijana katika shughuli za maendeleo ya mchezo wa ngumi kimataifa.

Aliongeza kuwa kuteuliwa kwa miraji ni fahari kwa watanzania na kutaongeza mchango mkubwa wa kukuza vipaji kwa mabondia vijana waliopo nchini.

Ni muda mrefi sasa michezo wa ngumi za ridhaa na kulipwa imekosa muamko mzuri katika mataifa ya Afrika kutokana na kutokuwepo kwa wainuaji wazuri wa michezo hiyo.

0 comments:

Post a Comment