BROWN ABEBESHWA KILICHO CHAKE.

         

Kocha wa klabu ya Los Angeles Laker Mike Brown ametimuliwa kazi ya kuinoa timu hiyo ya kikapu baada ya kuanza vibaya msimu wa ligi ya NBA kule nchini Marekani.
Mike Brown alishindwa kuanza vema katika michuano hiyo baada ya kufungwa mechi nne za awali za ligi hiyo kubwa ya kikapu ulimwengu.
 Baada ya kufukuzwa Brown amewashukuru viongozi na wachezaji wa Lakers kwa ushirikiano alioupata kwa muda wote wa kazi aliyoifanya ndani ya Lakers.
Baada kufukuzwa kwa Brown kocha msaidizi wa timu hiyo Bernie Bickerstaff alikiongoza kikosi cha Lakers kwenye mchezo wa leo dhidi Warriors na kushinda kwa vikapu  111 kwa 77.

0 comments:

Post a Comment